Swali: Mapambano dhidi ya ISIS, mashirika ya mitandao na uongozi wa kisyria ni miongoni mwa Jihaad katika njia ya Allaah?
Jibu: Jihaad hii imetangazwa? Je, watu wamezungumzia kuhusu ISIS na ni wepi na kina nani wenye kuwasaidia? Je, wako dhidi ya Iraan, nchi ya Raafidhwah? Je, wako dhidi ya makafiri wengine? Je, wako dhidi ya Nusayriyyah, ambao pia wanaitwa “´Alawiyyah”? Kuna linalojulikana juu yao? Hatujajua kitu kilicho wazi kabisa ili tukaweza kujua mfumo walio nao. Kwani wao wanamfuata ash-Shaafi´iy, Abu Haniyfah, Maalik au Ahmad? Kwa nini wanadai kuwa ni dola ya Kiislamu? Ni nani aliyesema kuwa ni dola ya Kiislamu? Hii ni fitina waliyopata Ummah wa Kiislamu.
  • Mhusika: ´Allaamah Swaalih bin Muhammad al-Luhaydaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=148858 Tarehe: 1436-02-05/2014-11-27
  • Imechapishwa: 06/11/2016