Swali 425: Ni ipi ya mfungaji kujitia baridi kidogo?

Jibu: Mfungaji kujiweka baridi ni jambo linalofaa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akijimwagia maji kichwani mwake kwa sababu ya joto kali au kwa sababu ya kiu ilihali amefunga[1]. Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) alikuwa akiilowesha nguo yake kwa maji ilihali amefunga kwa ajili ya kupunguza ukali wa joto au kiu. Unyevunyevu hauathiri. Kwani maji hayafiki tumboni.

[1] Abu Daawuud (2365).

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Arkaan-il-Islaam, uk. 481
  • Imechapishwa: 12/05/2019