Ni ipi tofauti kati ya kichenguzi cha pili na cha kwanza?

Swali: Ni ipi tofauti kati ya kichenguzi cha pili na cha kwanza?

Jibu: Kichenguzi cha pili ni aina ya kichenguzi cha kwanza. Kichenguzi cha kwanza ni chenye kuenea na hichi ni maalum. Shaykh amekitilia umuhimu kwa sababu kimetokea kwa watu. Kuyaabudu makaburi, mawalii na waja wema ni jambo limetokea kwa watu kwa wingi. Ama kuabudu miti, mawe na vinginevyo, mara nyingi ni kwamba hakuna yeyote katika waislamu anayekubaliana nayo. Lakini kuyaabudu makaburi wako wengi ambao wanajinasibisha na Uislamu wanakubaliana nayo na wanayazingatia kuwa ni katika Uislamu. Kwa ajili hiyo ndio maana Shaykh amelitilia umuhimu na akalifanya kuwa ni maalum. Nayo ni katika aina ya kile cha kwanza. Lakini ndio uhalisia katika maisha ya wengi ambao wanajinasibisha… hatusemi waislamu, lakini tunasema ambao wanajinasibisha katika Uislamu.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Nawaaqidh-il-Islaam, uk. 76
  • Imechapishwa: 30/08/2018