Swali 1029: Ni ipi hukumu ya mwanamke kufunika uso wake kwa wasiokuwa Mahram zake?
Jibu: Sunnah za kinabii zimefahamisha juu ya ulazima wa mwanamke kufunika uso wake mbele ya wasiokuwa Mahram zake. Kutokana na Hadiyth ya ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ambaye amesimulia:
“Wapanda farasi wanaume walikuwa wakitupitia na sisi tuko kwenye Ihraam pamoja na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Wanapotujongelea, kila mmoja wetu anateremsha mavazi yake ya juu, Jilbaab, usoni mwake. Wanapokuwa wameshapita, tunajifunua tena.”
Dalili kutoka katika Qur-aan na Sunnah kuhusu mwanamke kufunika uso wake mbele ya wasiokuwa Mahram zake ni nyingi. Napendekeza kwako dada muislamu kusoma kitabu “al-Hijaab wal-Libaas fiys-Swalaah” cha Ibn Taymiyyah, kitabu “al-Hijaab” cha Shaykh ´Abdul-´Aziyz bin Baaz, kitabu “as-Swaarim al-Mash-huur ´alaa al-Muftiyniyna bis-Sufuur” cha Shaykh Hamuud at-Tuwayjiriy na kitabu “al-Hijaab”[1] cha Shaykh Swaalih bin ´Uthaymiyn. Vitabu hivi ndani yake mna yenye kutosheleza.
[1] Tazama https://firqatunnajia.com/category/makala/wanawake/mavazi-na-vipodozi/jumla-kuhusiana-na-vazi-la-mwanamke/al-hijaab/
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Mar´ah al-Muslimah, uk. 410
- Imechapishwa: 08/10/2019
Swali 1029: Ni ipi hukumu ya mwanamke kufunika uso wake kwa wasiokuwa Mahram zake?
Jibu: Sunnah za kinabii zimefahamisha juu ya ulazima wa mwanamke kufunika uso wake mbele ya wasiokuwa Mahram zake. Kutokana na Hadiyth ya ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ambaye amesimulia:
“Wapanda farasi wanaume walikuwa wakitupitia na sisi tuko kwenye Ihraam pamoja na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Wanapotujongelea, kila mmoja wetu anateremsha mavazi yake ya juu, Jilbaab, usoni mwake. Wanapokuwa wameshapita, tunajifunua tena.”
Dalili kutoka katika Qur-aan na Sunnah kuhusu mwanamke kufunika uso wake mbele ya wasiokuwa Mahram zake ni nyingi. Napendekeza kwako dada muislamu kusoma kitabu “al-Hijaab wal-Libaas fiys-Swalaah” cha Ibn Taymiyyah, kitabu “al-Hijaab” cha Shaykh ´Abdul-´Aziyz bin Baaz, kitabu “as-Swaarim al-Mash-huur ´alaa al-Muftiyniyna bis-Sufuur” cha Shaykh Hamuud at-Tuwayjiriy na kitabu “al-Hijaab”[1] cha Shaykh Swaalih bin ´Uthaymiyn. Vitabu hivi ndani yake mna yenye kutosheleza.
[1] Tazama https://firqatunnajia.com/category/makala/wanawake/mavazi-na-vipodozi/jumla-kuhusiana-na-vazi-la-mwanamke/al-hijaab/
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa al-Mar´ah al-Muslimah, uk. 410
Imechapishwa: 08/10/2019
https://firqatunnajia.com/ni-ipi-hukumu-ya-mwanamke-kufunika-uso-wake-kwa-wasiokuwa-mahram-zake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)