Ni ipi hukumu ya kupunguza nywele zinazozidi kwenye nyusi?

Swali: Ni ipi hukumu ya kupunguza nywele zinazozidi kwenye nyusi?

Jibu: Haijuzu kukata wala kupunguza nywele zinazozidi kwenye nyusi. Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

“Kwamba amemlaani mwenye kuchonga nyusi na mwenye kuchongwa nyusi.”

Wanazuoni wamebainisha kwamba (النمص) ni kule kukata kitu katika nyusi.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (10/51)
  • Imechapishwa: 07/08/2021