Swali 28: Ni hali zipi ambapo mtu anasujudu Sujuud ya kusahau kabla ya Tasliym na baada ya Tasliym?
Jibu: Sujuud ya kusahau inasujudiwa kabla ya Tasliym isipokuwa tu katika hali mbili:
1- Pale atapotoa Tasliym mapema kwa kupunguza Rak´ah moja au zaidi. Katika hali hii bora ni kuileta baada ya Tasliym. Dalili ya hilo ni Hadiyth ya Dhuul-Yadayn (Radhiya Allaahu ´anh).
2- Pale ambapo mtu atakuwa na dhana yenye nguvu. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Atapokuwa na mashaka mmoja wenu juu ya swalah yake, basi ajibidishe juu ya lile la sawa, akamilishe kitendo chake, kisha alete Tasliym na kusujudu Sujudu mbili.”[1]
Ameifanya Sujuud kuwa baada ya Tasliym. Hili ndio bora. Vinginevo Sujuud ya kusahau mtu anaileta kabla ya Tasliym.
[1] al-Bukhaariy (401) na Muslim (572).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ash-Sharh al-Mumtaaz, uk. 36
- Imechapishwa: 02/11/2018
Swali 28: Ni hali zipi ambapo mtu anasujudu Sujuud ya kusahau kabla ya Tasliym na baada ya Tasliym?
Jibu: Sujuud ya kusahau inasujudiwa kabla ya Tasliym isipokuwa tu katika hali mbili:
1- Pale atapotoa Tasliym mapema kwa kupunguza Rak´ah moja au zaidi. Katika hali hii bora ni kuileta baada ya Tasliym. Dalili ya hilo ni Hadiyth ya Dhuul-Yadayn (Radhiya Allaahu ´anh).
2- Pale ambapo mtu atakuwa na dhana yenye nguvu. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Atapokuwa na mashaka mmoja wenu juu ya swalah yake, basi ajibidishe juu ya lile la sawa, akamilishe kitendo chake, kisha alete Tasliym na kusujudu Sujudu mbili.”[1]
Ameifanya Sujuud kuwa baada ya Tasliym. Hili ndio bora. Vinginevo Sujuud ya kusahau mtu anaileta kabla ya Tasliym.
[1] al-Bukhaariy (401) na Muslim (572).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: ash-Sharh al-Mumtaaz, uk. 36
Imechapishwa: 02/11/2018
https://firqatunnajia.com/ni-hali-zipi-ambapo-mtu-anasujudu-sujuud-ya-kusahau-kabla-ya-tasliym-na-baada-ya-tasliym/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)