Ndoa ya mwanandoa mmoja asiyeswali ni yenye kutenguka

Swali: Ndoa ya mtu asiyeswali inatenguka kwa mke wake ambaye anaswali?

Jibu: Ikiwa anaacha Swalah kwa kukusudia, ndoa inatenguka. Akitubu na yeye mke bado yumo ndani ya eda, anarudi kwake. Akitoka ndani ya eda na akawa bado hajatubia, anatengana naye. Baada ya kutubia itatakiwa kufunga ndoa mpya.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (53) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/mo–1432-06-12.mp3
  • Imechapishwa: 16/11/2014