Leo kumejitokeza mapote ambayo wanatumia akili zao juu ya dalili za Qur-aan na Sunnah na wanapinga mfano wa Hadiyth kama hizi zinazozungumzia mambo yaliyofichikana, wanayapotosha na kuyafasiri kimakosa. Kwa mfano Hadiyth ya al-Masiyh ad-Dajjaal wameipinga na kusema kwamba haiingii katika akili timamu. Hadiyth ya Muusa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumpiga ngumi Malaika wa mauti na jicho lake kutoka wameifasiri kimakosa na kusema kwamba haiingii katika akili timamu. Vivyo hivyo wamefanya juu ya mambo yatayokuwa katika uwanja wa Qiyaamah na ndani ya kaburi.

  • Mhusika: Shaykh Swaalih bin ´Abdil-´Aziyz Aalish-Shaykh
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 118
  • Imechapishwa: 28/08/2020