Swali: Mimi naishi katika mji wa kikafiri na nataka kufanya Hijrah. Lakini naishi peke yangu na mama yangu na yeye hataki kufanya Hijrah. Wakati huo huo siwezi kumuacha mama yangu peke yake. Ni lipi la wajibu ninalotakiwa kufanya?

Jibu: Shikamana barabara na dini yako na uwe na subira naye na mtendee wema. Shikamana bara bara na dini yako mpaka pale Allaah atapokuwekea wepesi wa kufanya Hijrah.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (40) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1431-3-8.mp3
  • Imechapishwa: 20/08/2020