Nasaha kwa anayetaka kuoa zaidi ya mke mmoja

Swali: Ni zipi nasaha zako kwa mtu ambaye anataka kuoa mke zaidi ya mmoja?

Jibu: Afanye uadilifu. Amche Allaah na afanye uadilifu:

فَإِنْ خِفْتُمْ أَلَّا تَعْدِلُوا فَوَاحِدَةً

“Mkikhofu kwamba hamtoweza kufanya uadilifu, basi mmoja tu.”[1]

Uadilifu unakuwa katika matumizi, mavazi, makazi na malazi. Uadilifu unaweza kufanywa katika mambo haya mane.

[1] 04:03

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Liqaa’ al-Maftuuh fiy Masjid Qubaa’ http://alfawzan.af.org.sa/ar/node/17626
  • Imechapishwa: 01/04/2018