Swalah ya ´iyd ni Rak´ah mbili. Imamu atasoma kwa sauti ya juu. Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:
”Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akisoma kwa sauti katika swalah za ´iyd mbili na swalah ya kuomba mvua.”
Ameipokea ad-Daaraqutwniy.
Wanachuoni wameafikiana juu ya hilo na yapo mapokezi ambayo baadhi ya Salaf wameonelea kinyume. Kitendo cha waislamu kiliendelea katika hali hiyo.
Atasoma katika ya kwanza baada ya al-Faatihah atasoma Suurah ”al-A´laa”. Katika Rak´ah ya pili atasoma Suurah ”al-Ghaashiyah”. Samarah amesema:
”Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika swalah za ´iyd mbili alikuwa akisoma:
سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى
“Tukuza jina la Mola wako Aliye juu.”[1]
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ
“Je, imekujia hadisi ya kufunikiza?”[2]
Ameipokea Ahmad.
Au akisoma katika Rak´ah ya kwanza Suurat ”Qaaf” na ya pili Suurah ”al-Qamar.” Vilevile akisoma mfano wa hizo kwa mujibu wa ilivyopokelewa katika Athar ndio bora zaidi.”
[1] 87:01
[2] 88:01
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Mulakhaswsw-ul-Fiqh (01/274)
- Imechapishwa: 29/07/2020
Swalah ya ´iyd ni Rak´ah mbili. Imamu atasoma kwa sauti ya juu. Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:
”Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akisoma kwa sauti katika swalah za ´iyd mbili na swalah ya kuomba mvua.”
Ameipokea ad-Daaraqutwniy.
Wanachuoni wameafikiana juu ya hilo na yapo mapokezi ambayo baadhi ya Salaf wameonelea kinyume. Kitendo cha waislamu kiliendelea katika hali hiyo.
Atasoma katika ya kwanza baada ya al-Faatihah atasoma Suurah ”al-A´laa”. Katika Rak´ah ya pili atasoma Suurah ”al-Ghaashiyah”. Samarah amesema:
”Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika swalah za ´iyd mbili alikuwa akisoma:
سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى
“Tukuza jina la Mola wako Aliye juu.”[1]
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ
“Je, imekujia hadisi ya kufunikiza?”[2]
Ameipokea Ahmad.
Au akisoma katika Rak´ah ya kwanza Suurat ”Qaaf” na ya pili Suurah ”al-Qamar.” Vilevile akisoma mfano wa hizo kwa mujibu wa ilivyopokelewa katika Athar ndio bora zaidi.”
[1] 87:01
[2] 88:01
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Mulakhaswsw-ul-Fiqh (01/274)
Imechapishwa: 29/07/2020
https://firqatunnajia.com/namna-ya-swalah-ya-iyd-kwa-ufupi-ii/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)