Namna ya kisomo katika swalah ya usiku au Witr

Swali: Kisomo cha Qur-aan katika swalah ya usiku inakuwa kusoma kwa sauti au kimyakimya?

Jibu: Atazame kile ambacho kina manufaa zaidi kwake. Ikiwa anataka kuukimbiza usingizi bora kwake ni yeye kusoma kwa sauti. Ama pembezoni mwake kukiwa mtu ambaye anasoma au analala basi asisome kwa sauti ya juu.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (03) http://audio2.islamweb.net/lecturs/aalrrajhee/430/430.mp3
  • Imechapishwa: 22/06/2018