Nilimsikia babangu na Abu Zur´ah wakiamrisha kuwasusa Ahl-ul-Bid´ah wapindaji. Walikuwa wakali katika hilo.

Walikuwa wakikemea kutunga vitabu kwa maoni pasi na mapokezi.

Walikuwa wakikataza kukaa na watu wa falsafa na kusoma vitabu vyao na kusema:

“Watu wa falsafa kamwe hawatofaulu.”

Na mimi nasema vivyo hivyo.

Abu ´Aliy bin Hubaysh al-Muqriy amesema:

“Na mimi nasema vivyo hivyo.”

Shaykh wetu Ibn-ul-Mudhaffar amesema:

“Na mimi nasema vivyo hivyo.”

Shaykh wetu amesema:

“Hali kadhalika ndivyo ninavyosema.”

  • Mhusika: Imaam Abu Muhammad ´Abdur-Rahmaan bin Haatim ar-Raaziy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ´Aqiydat-ur-Raaziyayn, uk. 223
  • Imechapishwa: 06/09/2020