Swali: Mimi ni mzee niliye na miaka themanini ambaye niko na maradhi kwenye mshipa na maradhi ya moyo. Sikuweza kufunga Ramadhaan ya mwaka 1404 uliyopita. Nimetoa mifuko mitatu kwa familia tatu zinazohitajia zinazopatikana katika kijiji chetu. Jumla ya hiyo mifuko mitatu ni Mudd[1] thelathini na nne. Mwaka huu pia sijui kama naweza kufunga au siwezi. Kwa ajili hiyo naomba mnipe fatwa kwa yale niliyokuelezeni kwa kuwa mimi sina amani isipokuwa baada ya kupata fatwa yenu.
Jibu: Mambo yakiwa kama ulivyotaja ya kwamba una miaka themanini na kwamba una maradhi ya kwenye mshipa na ya moyo na kuwa Ramadhaan iliyopita uliacha kufunga kwa sababu ya kutoweza kufunga, hakuna neno kula. Inatosheleza kulisha masikini mmoja kwa kila siku moja uliyoacha kufunga. Kiwango chake ni nusu pishi ambayo kiasi chake ni takriban 1,5 kg katika mchele, ngano na vyakula vyengine ambavyo vimezoeleka katika nchi yenu.
[1] Imaam ´Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: ”Mudd ni sawa na kama robo hivo.” (Sharh al-´Aqiydah al-Waasitwiyyah (02/252) iliyochapishwa na Daar Ibn-ul-Jawziy).
- Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (10/166-167)
- Imechapishwa: 04/06/2017
Swali: Mimi ni mzee niliye na miaka themanini ambaye niko na maradhi kwenye mshipa na maradhi ya moyo. Sikuweza kufunga Ramadhaan ya mwaka 1404 uliyopita. Nimetoa mifuko mitatu kwa familia tatu zinazohitajia zinazopatikana katika kijiji chetu. Jumla ya hiyo mifuko mitatu ni Mudd[1] thelathini na nne. Mwaka huu pia sijui kama naweza kufunga au siwezi. Kwa ajili hiyo naomba mnipe fatwa kwa yale niliyokuelezeni kwa kuwa mimi sina amani isipokuwa baada ya kupata fatwa yenu.
Jibu: Mambo yakiwa kama ulivyotaja ya kwamba una miaka themanini na kwamba una maradhi ya kwenye mshipa na ya moyo na kuwa Ramadhaan iliyopita uliacha kufunga kwa sababu ya kutoweza kufunga, hakuna neno kula. Inatosheleza kulisha masikini mmoja kwa kila siku moja uliyoacha kufunga. Kiwango chake ni nusu pishi ambayo kiasi chake ni takriban 1,5 kg katika mchele, ngano na vyakula vyengine ambavyo vimezoeleka katika nchi yenu.
[1] Imaam ´Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: ”Mudd ni sawa na kama robo hivo.” (Sharh al-´Aqiydah al-Waasitwiyyah (02/252) iliyochapishwa na Daar Ibn-ul-Jawziy).
Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (10/166-167)
Imechapishwa: 04/06/2017
https://firqatunnajia.com/mzee-ameshindwa-kufunga-kwa-sababu-ya-utuuzima-na-maradhi-sugu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)