Mwenye kuhiji kapita Miyqaat amevaa nguo za kawaida

Swali: Allaah anilijaalia mwaka ujao nikaweza kuhiji. Lakini ili niweze kuwakwepa polisi nilipita Miyqaat na huku nimevaa mavazi ya kawaida. Je, ni lazima kwangu kutoa kafara au fidia?

Jibu: Ndio. Ulipita Miyqaat na huku umevaa mavazi ya kawaida na pasi na Ihraam na wewe unanuia kuhiji. Ni lazima kwako kutoa fidia. Kwa sababu haya ni makatazo miongoni mwa makatazo ya Ihraam.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (90) https://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/%D8%A5%D8%BA%D8%A7%D8%AB%D8%A9%20%D8%A7%D9%84%D9%84%D9%87%D9%81%D8%A7%D9%86%20-15-07-1439.lite__0_0.mp3
  • Imechapishwa: 18/08/2018