Mwanamke kuomba talaka kwa mume anayetazama filamu za haramu

Swali: Mwanamke huyu anasema kuwa mume wake anatazama filamu za haramu. Nimemwita katika tawbah na amekariri tendo hili mpaka nimekuwa ninamchukia. Je, inajuzu kwangu kuomba kutengana naye katika hali hii?

Jibu: Ndio. Ikiwa hatubii na anazifuatilia, tendo hili linazingatiwa ni khatari katika heshima yake na heshima ya mke wake. Ukimuomba kutengana naye kwa hakimu, hakimu ndiye ambaye atasimamia hili.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/fth-mjd-17051435.mp3
  • Imechapishwa: 20/09/2020