Swali: Dhahabu anayotumia mwanamke anatakiwa kuitolea zakaah hata kama hana pesa ya kuitolea zakaah wala haweki akiba katika mshahara wake wa kila mwezi?
Jibu: Maoni sahihi ni kwamba anatakiwa kuitolea zakaah pale inapofikisha kile kiwango cha lazima. Wanazuoni wamekhitilafiana. Maoni sahihi ni kwamba inatolewa zakaah. Dhahabu na fedha – ni mamoja vinatumiwa au havitumiwi – vinatakiwa kutolewa zakaah kwa ambaye anavimiliki katika wanamme au wanawake pale vinapofikisha kile kiwango cha lazima. Kiwango cha lazima ni mithqaal 20 ambapo ni 92 g. Dhahabu inapofikisha kiwango hicho basi ni lazima kuitolea zakaah. Haijalishi kitu anaitumia au haitumii. Hukumu ni moja.
Kuhusu almasi na mawe mengine ya thamani ambayo yanatumiwa hayatolewi zakaah. Isipokuwa ikiwa yameandaliwa kwa ajili ya biashara.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/4420/حكم-ومقدار-زكاة-الحلي-المعد-للزينة
- Imechapishwa: 17/06/2022
Swali: Dhahabu anayotumia mwanamke anatakiwa kuitolea zakaah hata kama hana pesa ya kuitolea zakaah wala haweki akiba katika mshahara wake wa kila mwezi?
Jibu: Maoni sahihi ni kwamba anatakiwa kuitolea zakaah pale inapofikisha kile kiwango cha lazima. Wanazuoni wamekhitilafiana. Maoni sahihi ni kwamba inatolewa zakaah. Dhahabu na fedha – ni mamoja vinatumiwa au havitumiwi – vinatakiwa kutolewa zakaah kwa ambaye anavimiliki katika wanamme au wanawake pale vinapofikisha kile kiwango cha lazima. Kiwango cha lazima ni mithqaal 20 ambapo ni 92 g. Dhahabu inapofikisha kiwango hicho basi ni lazima kuitolea zakaah. Haijalishi kitu anaitumia au haitumii. Hukumu ni moja.
Kuhusu almasi na mawe mengine ya thamani ambayo yanatumiwa hayatolewi zakaah. Isipokuwa ikiwa yameandaliwa kwa ajili ya biashara.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/4420/حكم-ومقدار-زكاة-الحلي-المعد-للزينة
Imechapishwa: 17/06/2022
https://firqatunnajia.com/mwanamke-anatakiwa-kuyatolea-mapambo-yake-ya-dhahabu-na-fedha/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)