Swali: Kuna mwanaume ameoa mke wa pili ambapo mke wa kwanza akaanza kumtukana na kumlaani na kuomba du´aa dhidi yake na kila aliyeunga, aliyehudhuria au kuridhia ndoa hiyo, sawa awe ni ndugu au mtu mwingine. Mwanaume huyu ataamiliane naye vipi akiendelea katika hali hii?

Jibu: Ima awe na uvumilivu kwake mpaka pale ataponyooka ma kutengemaa au amtaliki. Ikiwa hawezi kumvumilia amtaliki ili astarehe naye.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Duruus-ul-Haram http://www.alfawzan.af.org.sa/node/14725
  • Imechapishwa: 03/05/2018