Swali: Mwanamke akiwa na deni la Ramadhaan inafaa kwake akatanguliza siku sita za Shawwaal kabla ya deni au deni la Ramadhaan kabla ya siku sita za Shawwaal?
Jibu: Mwanamke asifunge siku sita za Shawwaal akiwa yuko na deni la Ramadhaan kabla ya kumaliza kulipa deni lake. Kwani Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayefunga Ramadhaan kisha akaifuatishia siku sita za Shawwaal basi ni kama ambaye amefunga mwaka mzima.”
Yule mwenye deni la Ramadhaan hazingatiwi kuwa ameifunga Ramadhaan. Hivyo hapati thawabu za kufunga siku sita za Shawwaal isipokuwa baada ya kumaliza kulipa deni lake.
Lau tutakadiria kuwa ulipaji umechukua Shawwaal nzima, kwa mfano mwanamke hakufunga siku hata moja ya Ramadhaan kwa sababu alikuwa na damu ya uzazi Ramadhaan nzima, kisha akaanza kufunga siku sita za Shawwaal na asimalize isipokuwa baada ya kuingia Dhul-Qa´dah, ana ruhusa ya kufanya hivo. Analipwa thawabu za siku sita za Shawwaal kwa sababu alichelewesha kwa sababu ya dharurah na udhuru. Hivyo atalipwa ujira.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (20/19)
- Imechapishwa: 07/06/2019
Swali: Mwanamke akiwa na deni la Ramadhaan inafaa kwake akatanguliza siku sita za Shawwaal kabla ya deni au deni la Ramadhaan kabla ya siku sita za Shawwaal?
Jibu: Mwanamke asifunge siku sita za Shawwaal akiwa yuko na deni la Ramadhaan kabla ya kumaliza kulipa deni lake. Kwani Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayefunga Ramadhaan kisha akaifuatishia siku sita za Shawwaal basi ni kama ambaye amefunga mwaka mzima.”
Yule mwenye deni la Ramadhaan hazingatiwi kuwa ameifunga Ramadhaan. Hivyo hapati thawabu za kufunga siku sita za Shawwaal isipokuwa baada ya kumaliza kulipa deni lake.
Lau tutakadiria kuwa ulipaji umechukua Shawwaal nzima, kwa mfano mwanamke hakufunga siku hata moja ya Ramadhaan kwa sababu alikuwa na damu ya uzazi Ramadhaan nzima, kisha akaanza kufunga siku sita za Shawwaal na asimalize isipokuwa baada ya kuingia Dhul-Qa´dah, ana ruhusa ya kufanya hivo. Analipwa thawabu za siku sita za Shawwaal kwa sababu alichelewesha kwa sababu ya dharurah na udhuru. Hivyo atalipwa ujira.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (20/19)
Imechapishwa: 07/06/2019
https://firqatunnajia.com/mwanamke-amechelewesha-shawwaal-kwa-sababu-ya-udhuru-wa-kishariah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)