Swali: Ni jambo la aula zaidi mwanafunzi anayeanza ajifunze elimu ya misingi ya kuwaraddi wenye kwenda kinyume? Unamnasihi nini mwanafunzi anayeanza juu ya Ruduud hizi?

Jibu: Mwanafunzi anayeanza aanze kusoma vitabu vidogo vidogo kwa wanachuoni. Hivyo ndio funguo za elimu. Avisome kwa wanachuoni ambao watambainishia navyo na kumuwekea wazi. Aende hatua kwa hatua. Asikimbilie katika vitu vigumu na vitu ambavyo mwanzoni hawezi kuvifahamu.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Furqaan (14) http://alfawzan.af.org.sa/node/2057
  • Imechapishwa: 24/04/2017