Muunge ndugu yako japokuwa yeye amekukata

Swali: Je, niwaunge ndugu zangu ikiwa wananiudhi na ninachelea maudhi yao?

Jibu: Ndio, waunge ndugu zako hata kama wao watakukata. Hawatokudhuru – Allaah akitaka – bali ukiwaunga nyoyo zao zitalainika kwako. Ukiwakata ndio watazidi kukuchukia na kukukata zaidi. Muunge ndugu yako japokuwa yeye amekukata.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://alfawzan.af.org.sa/ar/node/17500
  • Imechapishwa: 21/11/2017