Swali: Wakati mwanamke mwenye kuhiji alipokuwa ´Arafah alijiwa na khabari kwamba mume wake kafariki. Ni kipi anachotakiwa kufanya?

Jibu: Anatakiwa kukamilisha hajj yake. Aidha anatakiwa kujiepusha na vitu vyenye harufu, mapambo na vitu vyengine vyote vinavyofungamana na hukumu za eda. Pindi ataporudi katika mji wake atatakiwa kukaa katika nyumba ileile alipokufia mume wake. Ataikamilisha eda yake nyumbani.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (23) https://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/Umdah-13-2-1435-01.mp3
  • Imechapishwa: 12/06/2020