Swali: Inajuzu kwa muislamu kujiunga na swalah ya faradhi na huku ananuia Tahiyyat-ul-Masjid? Kwa mfano nimejiunga na wewe katika msikiti huu ilihali nimeshaswali kabla yenu inafaa kwangu kunuia kuwa ni Tahiyyat-ul-Masjid?
Jibu: Mtu akiingia msikitini na akaswali swalah ya faradhi inamtosheleza kutokamana na Tahiyyat-ul-Masjid. Hakuna haja ya kunuia Tahiyyat-ul-Masjid. Malengo ya Tahiyyat-ul-Masjid ni wewe usikae isipokuwa umeswali Rak´ah mbili hizi. Jambo hili linapatikana kwa kuswali swalah hii ya faradhi na Raatibah ya kabla ya swalah. Ikiwa utaingia msikitini baada ya adhaana ya Fajr na wewe hujaswali Rak´ah mbili za Raatibah na ukawa umeziswali wakati ulipoingia zinatosheleza kutokamana na Tahiyyat-ul-Masjid. Vivyo hivyo iwapo utaingia na ukawakuta watu wanaswali ambapo ukajiunga nao inakutosheleza kutokamana na kuswali Tahiyyat-ul-Masjid. Kujiunga na watu walio wanaswali ni sunnah, kama alivyosema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipokuwa anawakhutubia wanaume wawili:
“Mtaposwali majumbani mwenu kisha mkaja msikitini mkakuta watu wanaswali mkusanyiko, swalini pamoja nao. Hakika kwenu itakuwa ni sunnah.”
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (31) http://binothaimeen.net/content/704
- Imechapishwa: 03/11/2017
Swali: Inajuzu kwa muislamu kujiunga na swalah ya faradhi na huku ananuia Tahiyyat-ul-Masjid? Kwa mfano nimejiunga na wewe katika msikiti huu ilihali nimeshaswali kabla yenu inafaa kwangu kunuia kuwa ni Tahiyyat-ul-Masjid?
Jibu: Mtu akiingia msikitini na akaswali swalah ya faradhi inamtosheleza kutokamana na Tahiyyat-ul-Masjid. Hakuna haja ya kunuia Tahiyyat-ul-Masjid. Malengo ya Tahiyyat-ul-Masjid ni wewe usikae isipokuwa umeswali Rak´ah mbili hizi. Jambo hili linapatikana kwa kuswali swalah hii ya faradhi na Raatibah ya kabla ya swalah. Ikiwa utaingia msikitini baada ya adhaana ya Fajr na wewe hujaswali Rak´ah mbili za Raatibah na ukawa umeziswali wakati ulipoingia zinatosheleza kutokamana na Tahiyyat-ul-Masjid. Vivyo hivyo iwapo utaingia na ukawakuta watu wanaswali ambapo ukajiunga nao inakutosheleza kutokamana na kuswali Tahiyyat-ul-Masjid. Kujiunga na watu walio wanaswali ni sunnah, kama alivyosema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipokuwa anawakhutubia wanaume wawili:
“Mtaposwali majumbani mwenu kisha mkaja msikitini mkakuta watu wanaswali mkusanyiko, swalini pamoja nao. Hakika kwenu itakuwa ni sunnah.”
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (31) http://binothaimeen.net/content/704
Imechapishwa: 03/11/2017
https://firqatunnajia.com/mtu-kunuia-tahiyyat-ul-masjid-na-mkusanyiko-unaoswali-faradhi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)