Swali: Kufanya I´tikaaf nje ya Ramadhaan ni jambo limewekwa katika Shari´ah?
Jibu: Lililowekwa katika Shari´ah ni kukaa I´tikaaf katika Ramadhaan peke yake. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakufanya I´tikaaf kwa isiyokuwa Ramadhaan mbali na Shawwaal. Sababu ilikuwa kwamba Ramadhaan moja wapo aliacha kufanya I´tikaaf ndipo akawa amefanya katika Shawwaal. Lakini endapo mtu atafanya I´tikaaf katika mwezi mwingine mbali na Ramadhaan itakuwa ni jambo lenye kujuzu. Kwa sababu ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kusema:
“Mimi niliweka nadhiri kukaa I´tikaaf usiku au mchana katika msikiti Mtakatifu.” Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Tekeleza nadhiri yako.”
Lakini hata hivyo mtu hakuamrishwa na wala haikupendekezwa kwake kufanya I´tikaaf katika mwezi mwingine usiokuwa Ramadhaan.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (20/159-160)
- Imechapishwa: 15/06/2017
Swali: Kufanya I´tikaaf nje ya Ramadhaan ni jambo limewekwa katika Shari´ah?
Jibu: Lililowekwa katika Shari´ah ni kukaa I´tikaaf katika Ramadhaan peke yake. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakufanya I´tikaaf kwa isiyokuwa Ramadhaan mbali na Shawwaal. Sababu ilikuwa kwamba Ramadhaan moja wapo aliacha kufanya I´tikaaf ndipo akawa amefanya katika Shawwaal. Lakini endapo mtu atafanya I´tikaaf katika mwezi mwingine mbali na Ramadhaan itakuwa ni jambo lenye kujuzu. Kwa sababu ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kusema:
“Mimi niliweka nadhiri kukaa I´tikaaf usiku au mchana katika msikiti Mtakatifu.” Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Tekeleza nadhiri yako.”
Lakini hata hivyo mtu hakuamrishwa na wala haikupendekezwa kwake kufanya I´tikaaf katika mwezi mwingine usiokuwa Ramadhaan.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (20/159-160)
Imechapishwa: 15/06/2017
https://firqatunnajia.com/mtu-anaweza-kufanya-itikaaf-katika-mwezi-mwingine-mbali-na-ramadhaan/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)