Mswaliji anakata nia katikati ya swalah

Swali: Ni ipi hukumu mtu akikata nia yake katikati ya swalah?

Jibu: Mswaliji akikata nia katikati ya swalah basi swalah yake inabatilika. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Hakika kila kitendo kinategemea nia na kila mmoja atalipwa kwa kile alichonuia.”

Huyu amenuia kuikata na hivyo inakatika.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/450
  • Imechapishwa: 05/08/2017