Swali: Mimi ni msafiri na sijaswali Maghrib wala ´Ishaa. Nikaingia msikitini na wao ndio wanaanza kuswali ´Ishaa. Nikajichelewesah Rak´ah moja katika swalah ya ´Ishaa na nikakamilisha zilizobaki kwa nia ya Maghrib. Ndugu mmoja ananikataza na kwamba eti kitendo changu kinapingana na Sunnah na kwamba ni kosa. Ni yepi maoni yako juu ya swalah yangu?
Jibu: Mtu akija hali ya kuwa ni msafiri na akaingia msikitini akakuta watu wanaswali ´Ishaa, akiwakuta katika Rak´ah ya pili basi anuie Maghrib na atoe Tasliym pamoja na imamu. Kwa sababu katika hali hiyo atakuwa ameswali Rak´ah tatu. Akiwakuta katika Rak´ah ya tatu, anuie Maghrib na kuswali pamoja nao Rak´ah mbili kisha imamu akitoa Tasliym asimame katika Rak´ah ya tatu. Akijiunga nao katika Rak´ah ya kwanza aingie nao kwa kunuia Maghrib. Pindi imamu ataposimama kwa ajili ya Rak´ah ya nne basi yeye abaki chini na anuie kujitenga, asome Tashahhud, atoe Tasliym kisha ajiunge pamoja na imamu katika yale yatayokuwa yamebaki katika swalah ya ´Ishaa.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (49) http://binothaimeen.net/content/1127
- Imechapishwa: 01/05/2019
Swali: Mimi ni msafiri na sijaswali Maghrib wala ´Ishaa. Nikaingia msikitini na wao ndio wanaanza kuswali ´Ishaa. Nikajichelewesah Rak´ah moja katika swalah ya ´Ishaa na nikakamilisha zilizobaki kwa nia ya Maghrib. Ndugu mmoja ananikataza na kwamba eti kitendo changu kinapingana na Sunnah na kwamba ni kosa. Ni yepi maoni yako juu ya swalah yangu?
Jibu: Mtu akija hali ya kuwa ni msafiri na akaingia msikitini akakuta watu wanaswali ´Ishaa, akiwakuta katika Rak´ah ya pili basi anuie Maghrib na atoe Tasliym pamoja na imamu. Kwa sababu katika hali hiyo atakuwa ameswali Rak´ah tatu. Akiwakuta katika Rak´ah ya tatu, anuie Maghrib na kuswali pamoja nao Rak´ah mbili kisha imamu akitoa Tasliym asimame katika Rak´ah ya tatu. Akijiunga nao katika Rak´ah ya kwanza aingie nao kwa kunuia Maghrib. Pindi imamu ataposimama kwa ajili ya Rak´ah ya nne basi yeye abaki chini na anuie kujitenga, asome Tashahhud, atoe Tasliym kisha ajiunge pamoja na imamu katika yale yatayokuwa yamebaki katika swalah ya ´Ishaa.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (49) http://binothaimeen.net/content/1127
Imechapishwa: 01/05/2019
https://firqatunnajia.com/msafiri-kuswali-maghrib-nyuma-ya-anayeswali-ishaa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)