Swali: Je, inajuzu kwa mtu aliyenuia safari kula kabla hajatoka nyumbani kwake? Ikiwa inajuzu ni ipi hukumu ikiwa atanuia safari na akala kabla ya kutoka halafu asisafiri tena?
Jibu: Haijuzu kwa mwenye kunuia safari kula mpaka atoke katika mji. Hilo ni kwa kuwa rukhusa za safari zimefungamana na kupatikana kwa safari kimatendo. Kwa kuwa Allaah (Ta´ala) amesema:
وَإِذَا ضَرَبْتُمْ فِي الْأَرْضِ فَلَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ أَن تَقْصُرُوا مِنَ الصَّلَاةِ
“Mtakaposafiri katika ardhi, basi si dhambi kwenu kufupisha Swalaah.” (04:101)
Amesema “mtakaposafiri” na Hakusema “mtakapotaka”. Neno “kusafiri” inakuwa kwa kutoka katika mji. Haijuzu kwa anayenuia safari kula isipokuwa mpaka pale ataposafiri kimatendo.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kanda “Liqaa´aatu Ramadhwaaniyyah”, sehemu ya 02
- Imechapishwa: 23/09/2020
Swali: Je, inajuzu kwa mtu aliyenuia safari kula kabla hajatoka nyumbani kwake? Ikiwa inajuzu ni ipi hukumu ikiwa atanuia safari na akala kabla ya kutoka halafu asisafiri tena?
Jibu: Haijuzu kwa mwenye kunuia safari kula mpaka atoke katika mji. Hilo ni kwa kuwa rukhusa za safari zimefungamana na kupatikana kwa safari kimatendo. Kwa kuwa Allaah (Ta´ala) amesema:
وَإِذَا ضَرَبْتُمْ فِي الْأَرْضِ فَلَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ أَن تَقْصُرُوا مِنَ الصَّلَاةِ
“Mtakaposafiri katika ardhi, basi si dhambi kwenu kufupisha Swalaah.” (04:101)
Amesema “mtakaposafiri” na Hakusema “mtakapotaka”. Neno “kusafiri” inakuwa kwa kutoka katika mji. Haijuzu kwa anayenuia safari kula isipokuwa mpaka pale ataposafiri kimatendo.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Kanda “Liqaa´aatu Ramadhwaaniyyah”, sehemu ya 02
Imechapishwa: 23/09/2020
https://firqatunnajia.com/msafiri-kula-ramadhaan-kabla-ya-kuanza-safari/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)