Msafiri anaswali kwa kukaa ilihali anaweza kusimama

532- Nilimsikia Ahmad bin Hanbal akiulizwa juu ya mtu ambaye anaswali juu ya meli kwa kukaa. Akasema:

“Ikiwa alikuwa anaweza kuswali kwa kusimama, basi naonelea kuwa airudi swalah yake.”

533- Nilimsikia Ahmad bin Hanbal akiulizwa juu ya mtu ambaye anaswali juu ya meli ambapo akajibu kwa kusema:

“Aswali kwa kusimama iwapo anaweza kufanya hivo.”

  • Mhusika: Imaam Abu Daawuud as-Sijistaaniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Masaa-il-ul-Imaam Ahmad, uk. 110
  • Imechapishwa: 06/07/2019