Swali: Wakati mtu anapooa na kukamilisha zile sharti zinazomlazimu kisha mwanaume anataka kumchukua mke wake mlezi wa mwanamke huyu anamkatalia. Vinginevyo anamuhudumia na harusiwi kwenda nyumbani kwake. Mwanaume anakuwa na kazi ya kwenda na kurudi nyumbani kwa baba yake mdogo ambaye ndiye mlezi wa msichana huyu. Mume akimwacha mke wake kwa sababu hii kwa muda mrefu kwa kujengea matakwa ya mke juu ya mumewe huenda mambo yakaisha anapata dhambi? Au kukitokea talaka kwa njia hii kwa sababu ya msimamizi wa mwanamke huyu mume anapata dhambi?

Jibu: Ikiwa baba alimuwekea sharti wakati wa ndoa au alikubaliana naye kabla ya ndoa kumwacha mke wake kwa baba yake, basi ni lazima kwake kutimiza sharti hii. Haifai kwake kuomba kumtoa nje ya nyumba ya baba yake. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Masharti ambayo ni wajibu zaidi kwenu kuyatimiza ni yale mliyofanyiwa halali kwa tupu zenu.”

Ikiwa hakumuwekea sharti kabla ya ndoa wala hawakukubaliana naye kwamba atabaki nyumbani kwa baba yake, basi mke atamfuata mume wake. Katika hali hii mwanaume ana haki ya kumchukua kutoka nyumbani kwake, kumlazimisha juu ya hilo na aishi pamoja naye.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Nuur ´alaad-Darb (15) http://binothaimeen.net/content/6802
  • Imechapishwa: 27/02/2021