Swali 807: Vipi ikiwa mwanamke na familia yake wakiweka sharti asitolewe nje ya nyumba yake wala mji wake?
Jibu: Mwanamke au walii wake akimuwekea sharti mwanaume kubaki katika mji wake na kutohama pamoja na mume wake kwenda mji mwingine ni sharti sahihi ambayo ni lazima kuitendea kazi. ´Uqbah bin ´Aamir amepokea ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Masharti ambayo ni wajibu zaidi kwenu kuyatimiza ni yale mliyofanyiwa halali kwa tupu zenu.”
al-Athram amepokea kwamba kuna mwanaume alimuoa mwanamke ambaye alimuwekea sharti ya kulazimiana na nyumba yake ambapo baadaye mwanaume akataka kumuhamisha. Wakaenda kwa ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) hali ya kuwa ni wenye kugombana ambapo akasema: “Ana haki ya kulazimiana na sharti yake. Lakini mke akitaka kuhama pamoja naye, ana haki ya kufanya hivo, na akitaka kuidondosha imedondoka.”
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Ibraahiym Aalush-Shaykh
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Mar´ah al-Muslimah, uk. 319
- Imechapishwa: 04/08/2019
Swali 807: Vipi ikiwa mwanamke na familia yake wakiweka sharti asitolewe nje ya nyumba yake wala mji wake?
Jibu: Mwanamke au walii wake akimuwekea sharti mwanaume kubaki katika mji wake na kutohama pamoja na mume wake kwenda mji mwingine ni sharti sahihi ambayo ni lazima kuitendea kazi. ´Uqbah bin ´Aamir amepokea ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Masharti ambayo ni wajibu zaidi kwenu kuyatimiza ni yale mliyofanyiwa halali kwa tupu zenu.”
al-Athram amepokea kwamba kuna mwanaume alimuoa mwanamke ambaye alimuwekea sharti ya kulazimiana na nyumba yake ambapo baadaye mwanaume akataka kumuhamisha. Wakaenda kwa ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) hali ya kuwa ni wenye kugombana ambapo akasema: “Ana haki ya kulazimiana na sharti yake. Lakini mke akitaka kuhama pamoja naye, ana haki ya kufanya hivo, na akitaka kuidondosha imedondoka.”
Mhusika: Imaam Muhammad bin Ibraahiym Aalush-Shaykh
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa al-Mar´ah al-Muslimah, uk. 319
Imechapishwa: 04/08/2019
https://firqatunnajia.com/mke-ameshurutisha-asitolewe-nje-ya-mji-wake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)