Swali: Baadhi ya miji ndimi zao zimezowea kuapa kwa jina la Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Je, wakemewe kwa kuendelea na jambo hilo?

Jibu: Ndio. Wabainishieni kuwa kitendo hicho hakifai. Haifai kuapa kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hakuapwi isipokuwa kwa jina la Allaah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Mwenye kutaka kuapa basi aape kwa Allaah au anyamaze.”

“Msiape kwa baba zenu.”

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (107) https://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/ighatoulahfan-22-06-1441.mp3
  • Imechapishwa: 11/09/2020