460- Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Siku ya Qiyaamah Allaah hatomwangalia yule mtu ambaye anaiburuta nguo yake kwa kiburi.” Umm Salamah: ”Wanawake wafanye nini na mikia yao?” Akasema: ”Waburute shibiri moja.” Akasema: ”Basi nyayo zao (miguu yao) itaonekana.” Ndipo akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam): ”Basi waburute dhiraa moja.”
Ameipokea Abu Ya´laa katika ”al-Musnad”[1].
Cheni ya wapokezi ni Swahiyh. Wapokezi wake ni waaminifu na ni wanaume wa al-Bukhaariy na Muslim isipokuwa tu Ibraahiym bin al-Hajjaaj ambaye ni mwaminifu.
Katika Hadiyth kuna dalili inayoonyesha kuwa unyayo wa mwanamke ni ´Awrah, jambo ambalo lilikuwa linatambulika kwa wanawake wakati wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Wakati (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipowaambia: ”Waburute shibiri moja.” Umm Salamah akasema: ”Basi nyayo zao (miguu yao) itaonekana.” Ni jambo linaloashiria kwamba alikuwa akitambua kuwa nyayo za mwanamke ni ´Awrah na hazijuzu kuonekana. Kwa ajili hiyo ndio maana Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamwamrisha aburute urefu wa dhiraa moja. Qur-aan tukufu imeashiria hilo pale Allaah (Ta´ala) aliposema:
وَلَا يَضْرِبْنَ بِأَرْجُلِهِنَّ لِيُعْلَمَ مَا يُخْفِينَ مِن زِينَتِهِنَّ
“Wala wasipige miguu yao yakajulikana yale wanayoyaficha katika mapambo yao.”[2]
[1] 1/325.
[2] 24:31
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Silsilat-ul-Ahaadiyth as-Swahiyhah (1/2/827-828)
- Imechapishwa: 19/05/2019
460- Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Siku ya Qiyaamah Allaah hatomwangalia yule mtu ambaye anaiburuta nguo yake kwa kiburi.” Umm Salamah: ”Wanawake wafanye nini na mikia yao?” Akasema: ”Waburute shibiri moja.” Akasema: ”Basi nyayo zao (miguu yao) itaonekana.” Ndipo akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam): ”Basi waburute dhiraa moja.”
Ameipokea Abu Ya´laa katika ”al-Musnad”[1].
Cheni ya wapokezi ni Swahiyh. Wapokezi wake ni waaminifu na ni wanaume wa al-Bukhaariy na Muslim isipokuwa tu Ibraahiym bin al-Hajjaaj ambaye ni mwaminifu.
Katika Hadiyth kuna dalili inayoonyesha kuwa unyayo wa mwanamke ni ´Awrah, jambo ambalo lilikuwa linatambulika kwa wanawake wakati wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Wakati (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipowaambia: ”Waburute shibiri moja.” Umm Salamah akasema: ”Basi nyayo zao (miguu yao) itaonekana.” Ni jambo linaloashiria kwamba alikuwa akitambua kuwa nyayo za mwanamke ni ´Awrah na hazijuzu kuonekana. Kwa ajili hiyo ndio maana Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamwamrisha aburute urefu wa dhiraa moja. Qur-aan tukufu imeashiria hilo pale Allaah (Ta´ala) aliposema:
وَلَا يَضْرِبْنَ بِأَرْجُلِهِنَّ لِيُعْلَمَ مَا يُخْفِينَ مِن زِينَتِهِنَّ
“Wala wasipige miguu yao yakajulikana yale wanayoyaficha katika mapambo yao.”[2]
[1] 1/325.
[2] 24:31
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Silsilat-ul-Ahaadiyth as-Swahiyhah (1/2/827-828)
Imechapishwa: 19/05/2019
https://firqatunnajia.com/miguu-ya-mwanamke-ni-awrah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)