Mfungwa gerezani vipi atatia wudhuu´?

Swali: Mtu afanye nini akiwa gerezani na asipate maji wala udongo na wakati wa swalah ukawa unakaribia kutoka?

Jibu: Aswali kama alivyo. Asipopata maji, hakuna yeyote awezae kumletea maji na wala asipate udongo… atazame kwenye ukuta au kwenye mkeka ikiwa atapata vumbi. Akipata vumbi inamtosha kwake akapiga mikono yake mipigo miwili kisha akafuta mara moja usoni mwake na kwenye vitanga vyake vya mikono. Asipopata kitu basi aswali alivyo. Hili khaswa khaswa pale ambapo inahusiana na zile swalah ambazo mtu hawezi kuzikusanya na zengine.

  • Mhusika: Shaykh Muhammad bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://mdkhly.com/1427
  • Imechapishwa: 25/11/2017