Swali: Je, inajuzu kwa mlinganizi kusema:
“Ee Allaah! Hakika mimi nakuomba kwa majina na sifa Zako kuu.”?
Je, du´aa hii huku ni kuiomba sifa?
Jibu: Nakuomba kwa majina mazuri kabisa na sifa Zako kuu, huku ni kutawassul kwa Allaah kwa majina na sifa Zako. Sio kuomba sifa. Ni kumuomba Allaah. Amesema (Ta´ala):
وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ وَذَرُوا الَّذِينَ يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ ۚ سَيُجْزَوْنَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ
”Allaah ana majina mazuri kabisa. Hivyo basi, muombeni kwayo. Waacheni wale wanaopotoa/haribu katika majina Yake. Watalipwa yale waliyokuwa wakiyatenda.” (al-A´raaf 07:180)
Hiyo “kwa” (باء) ni Tawassul. Ni kama mfano wa:
“Kwa rehema Zako nakuomba msaada.”
Hii ni Hadiyth.
Swali: Ni upi mfano uliokatazwa wa kuomba sifa ya Allaah?
Jibu: Kama vile kusema “Ee uso wa Allaah!”, “Ee rehema za Allaah!” na mfano wake.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Nawaaqidh-il-Islaam, uk. 77
- Imechapishwa: 23/02/2019
Swali: Je, inajuzu kwa mlinganizi kusema:
“Ee Allaah! Hakika mimi nakuomba kwa majina na sifa Zako kuu.”?
Je, du´aa hii huku ni kuiomba sifa?
Jibu: Nakuomba kwa majina mazuri kabisa na sifa Zako kuu, huku ni kutawassul kwa Allaah kwa majina na sifa Zako. Sio kuomba sifa. Ni kumuomba Allaah. Amesema (Ta´ala):
وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ وَذَرُوا الَّذِينَ يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ ۚ سَيُجْزَوْنَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ
”Allaah ana majina mazuri kabisa. Hivyo basi, muombeni kwayo. Waacheni wale wanaopotoa/haribu katika majina Yake. Watalipwa yale waliyokuwa wakiyatenda.” (al-A´raaf 07:180)
Hiyo “kwa” (باء) ni Tawassul. Ni kama mfano wa:
“Kwa rehema Zako nakuomba msaada.”
Hii ni Hadiyth.
Swali: Ni upi mfano uliokatazwa wa kuomba sifa ya Allaah?
Jibu: Kama vile kusema “Ee uso wa Allaah!”, “Ee rehema za Allaah!” na mfano wake.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Nawaaqidh-il-Islaam, uk. 77
Imechapishwa: 23/02/2019
https://firqatunnajia.com/mfano-wa-kuomba-sifa-ya-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)