Mfano juu ya uongo wa Ibn Batwuutah juu ya Ibn Taymiyyah

Imesimuliwa kutoka kwa baadhi ya watu wajinga wakiuliza ni vipi mbingu zinakuwa wakati Allaah anaposhuka. Wakasema:

“Huzinyanyua kisha huzishusha. Yeye ni muweza wa kufanya hivo.”

Kila ambaye anafikiria yale ambayo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amemsifu Mola wake ni kama sifa za viwiliwili vyao ni wenye kupotea. Kisha baada ya hapo wanajigawanya makundi mawili.

  • Mhusika: Shaykh-ul-Islaam Ahmad bin Taymiyyah
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Hadiyth-in-Nuzuul, uk. 113
  • Imechapishwa: 01/04/2019