Swali: Kunaenezwa meseji zinazohusiana na kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na ndani yake mna yafuatayo:

“Ninakuomba kutokana na utukufu wa Allaah uwatumie wengine.”

Je, ni lazima kwangu kuituma?

Jibu: Hapana. Kitendo hichi hakina asli. Simu leo zinatumiwa kueneza Bid´ah, ima kwa kukusudia au pasi na kukusudia. Haijuzu kufanyia kazi yale yenye kuenezwa katika simu.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Tafsiyr-ish-Shaykh Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (13) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1432-08-09.mp3
  • Imechapishwa: 08/06/2020