Mwanamke ambaye ataposwa kwa yule mwanaume atakayemposa ni kama mwanamke wa kawaida wa sokoni. Si halali kwake kustarehe naye kwa kitu chochote. Hili linatupelekea katika kutaja jambo fulani; baadhi ya wanaume wanapomposa mwanamke wanazungumza naye kwenye simu maneno mengi. Hali imefikia kiasi cha kwamba nimefikiwa na khabari ya kwamba baadhi yao wanakesha usiku mzima na huku wanazungumza. Haya yametufikia. Hili ni jambo la haramu. Mwanamke huyu kwa hivi sasa ni mke wake au si mke wake? Si mke wake. Ni vipi ataweza kuzungumza naye na matamanio yake yasitikisike? Hili ni jambo gumu kuepukika. Baadhi ya watu wanasema kuwa wanazungumza naye ili kujua utamadukani alionao. Utapoishi naye ndipo utamjaribu. Ama kwa hivi sasa bado ni mwanamke ajinabi kwako. Yeye si halali kwako wala wewe si halali kwake.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (46) hhttp://binothaimeen.net/content/1055
- Imechapishwa: 11/03/2019
Mwanamke ambaye ataposwa kwa yule mwanaume atakayemposa ni kama mwanamke wa kawaida wa sokoni. Si halali kwake kustarehe naye kwa kitu chochote. Hili linatupelekea katika kutaja jambo fulani; baadhi ya wanaume wanapomposa mwanamke wanazungumza naye kwenye simu maneno mengi. Hali imefikia kiasi cha kwamba nimefikiwa na khabari ya kwamba baadhi yao wanakesha usiku mzima na huku wanazungumza. Haya yametufikia. Hili ni jambo la haramu. Mwanamke huyu kwa hivi sasa ni mke wake au si mke wake? Si mke wake. Ni vipi ataweza kuzungumza naye na matamanio yake yasitikisike? Hili ni jambo gumu kuepukika. Baadhi ya watu wanasema kuwa wanazungumza naye ili kujua utamadukani alionao. Utapoishi naye ndipo utamjaribu. Ama kwa hivi sasa bado ni mwanamke ajinabi kwako. Yeye si halali kwako wala wewe si halali kwake.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (46) hhttp://binothaimeen.net/content/1055
Imechapishwa: 11/03/2019
https://firqatunnajia.com/mazungumzo-kati-ya-wachumba/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)