Swali: Kuweka maandishi kama “Ametakasika Allaah” (سبحان الله), “Himdi zote ni za Allaah” (الحمد لله) na “Mdhukuru Allaah” (اذكر الله) kwenye gari inazingatiwa ni hirizi?

Jibu: Inazingatiwa ni hirizi. Haijuzu kuandika Aayah za Qur-aan, Hadiyth au du´aa kwenye magari. Haya ni matendo ya wajinga. Haijuzu kufanya hivi na kitendo hichi kinaifanya kutwezwa.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Fath-il-Majiyd (64) http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/28-07-1438h-fathou.mp3
  • Imechapishwa: 29/07/2017