Masomo ya Kiislamu kupitia mtandano

Swali: Mtu ambaye anasikiliza darsa za wanachuoni kupitia intaneti anaingia ndani ya ujumla wa maneno ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

“Yule ambaye atashika njia akitafuta ndani yake elimu, basi Allaah atamsahilishia njia ya kuelekea Peponi.”[1]?

Jibu: Ndio, anaingia ndani yake lakini hata hivyo hawezi kulinganishwa na wale wanaokaa chini ya wanachuoni, wakasafiri kwenda kwao na wakawasikiliza. Ana fungu lake katika fadhilah na thawabu, lakini si kama yule ambaye anakaa mbele yao, akawasikiliza, akawauliza na wakamjibu.

[1] Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (69).

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Fath-il-Majiyd (87) https://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/fathoumaged05-03-1440h.mp3
  • Imechapishwa: 27/04/2019