Swali: Inajuzu kwa Salafiyyuun kutumia fursa ya kupokea misaada inayotoka kwa Hizbiyyuun pamoja na kujua ya kwamba Hizbiyyuun hawatoi misaada hii isipokuwa wanachotaka ni kuwatumia Salafiyyuun?

Jibu: Ikiwa zawadi hizi ni kwa njia ya kuuza na kununua na kupakana mafuta juu ya ´Aqiydah, basi haijuzu kuzipokea. Ikiwa ni kwa sura hii basi haijuzu kuzipokea. Wao wanachukua mali za waislamu kwa ajili ya waislamu. Wakikupa pasi na kukuwekea sharti na wakati huohuo ukawa muhitaji pokea. Lakini kwa sharti asiuze dini yako. Lakini mara nyingi watu hawa wakipokea mali kutoka kwao wanaharibika. Muislamu akitaka kuilinda dini na ´Aqiydah yake basi avipe kisogo vile vilivyoko kwao na ajiweke mbali na wao na awe na subira juu ya ugumu wa maisha mpaka pale Allaah atapomfungulia.

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kanda: Liqaa´ As-ilah ma´ash-Shaykh Rabiy´ http://rabee.net/ar/questions.php?cat=29&id=287
  • Imechapishwa: 14/04/2018