Mapenzi baina ya wanandoa ni ya kimaumbile na sio ya kidini

Swali: Mapenzi ya mume kumpenda mke wake na kumwambia “Mimi siwezi kuishi bila ya wewe”, je, haya ni mapenzi ya kumpenda asiyekuwa Allaah na kujifungamanisha na asiyekuwa Yeye?

Jibu: Haya ni mapenzi ya kimaumbile:

وَجَعَلَ بَيْنَكُم مَّوَدَّةً وَرَحْمَةً

“Amekujaalieni baina yenu mapenzi na rehema.” (30:21)

Haya ni mapenzi ya kimaumbile na sio mapenzi ya ´Ibaadah. Hakuna neno kwayo.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/ighastah_09-11-1434_0.mp3
  • Imechapishwa: 20/09/2020