Mama anataka mke wangu aoneshe uso mbele ya ndugu zangu wa kiume

Swali: Mamangu bado ni mwenye kuendelea kumuomba mke wangu kuonesha uso wake mbele ya ndugu zangu ambao wamekwishabaleghe. Nimeshamnasihi mara nyingi ya kwamba hili halijuzu, lakini bado ameng´anga´ania kumuomba hili mke wangu. Unaninasihi nini katika jambo hili?

Jibu: Tunakunasihi kumuasi katika jambo hili. Haijuzu kwenu kumtii katika kumuasi Allaah (´Azza wa Jall).

“Hakuna utiifu kwa kiumbe katika kumuasi Muumba.”

Kiumbe yeyote yule. Hata baba hatiiwi katika kumuasi Allaah (´Azza wa Jall):

وَإِن جَاهَدَاكَ لِتُشْرِكَ بِي مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ فَلَا تُطِعْهُمَا

“Wakikufanyia juhudi kwamba unishirikishe na ambayo huna elimu nayo, basi usiwatii.” (29:08)

Haijuzu kumtii mzazi katika kumuasi Allaah (´Azza wa Jall), si mzazi wala mwengine yeyote.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/mntq–20041434.mp3
  • Imechapishwa: 19/09/2020