Makundi sabini na mbili yatadumishwa Motoni milele?

Swali: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Ummah wangu utafarikiana mapote sabini na tatu. Yote yataingia Motoni isipokuwa moja tu.”

Je, mapote yote haya yatadumishwa Motoni milele?

Jibu: Kinachotambulika kwa wanachuoni ni kwamba watu hawa ni miongoni mwa waliopewa matishio na kwamba ni katika wazushi. Kwa ajili hii wamesema kwamba Jahmiyyah ni wenye kutoka nje ya makundi haya sabini na mbili kwa sababu ni makafiri.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (10) https://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=FullContent&audioid=191426#219753
  • Imechapishwa: 13/05/2019