Swali: Kuhusu kuwaita mayahudi “waisraaiyl” na manaswara “wakristo” inahusiana na Tamyi´ kwa msingi kwamba watu wasiwachukie?

Jibu: Hapana, hizi ni istilahi baina yao. Wanaitwa ´wakristo` kwa sababu baadhi yao wanamwabudu al-Masiyh na ´Ahl-ul-Kitaab` kwa sababu wanajinasibisha katika Tawraat na Injiyl. Kilicho muhimu ni kwamba muumini asijinasibishe kwa mayahudi, manaswara wala kwa wale ambao wana kitu katika Bid´ah kama mfano wa Jahmiyyah na Mu´tazilah. Lengo ajiepushe na shari na watu wake. Badala yake anatakiwa kujinasibisha na Ahl-us-Sunnah, Maswahabah na wale waliofuata mwenendo wao imara ambao ni as-Salaf as-Swaalih.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Kashf-ish-Shubuhaat, uk. 18
  • Imechapishwa: 22/02/2019