Makalio na sehemu ya mgongo ya mswaliji inaonekana

Swali: Baadhi ya wanaoswali na suruwali wanaposujudu maumbile ya makalio yao na sehemu ya mgongo yao inaonekana. Je, tuwaamrishe kuzirudi swalah zao?

Jibu: Hapana, hawakujua hilo. Msiwaamrishe kuzirudi ikiwa hawakujua hilo. Hawakukusudia kufanya hivo. Badala yake wabainishieni na waambie wavae mavazi mazuri ili kifunikike kilichoko baina ya kitovu na magoti. Wazindueni juu ya hilo, lakini msiwaambie kuwa swalah zao ni batili.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (8) http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/umdt–14340429.mp3
  • Imechapishwa: 25/01/2017