Swali: Mwenye kupeleka maana ya “Laa ilaaha illa Allaah” katika Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah na al-Haakimiyyah anazingatiwa ni miongoni mwa wale ambao makafiri wa ki-Quraysh ni wenye ufahamu zaidi yake?
Jibu: Bila ya shaka yoyote. Makafiri wa ki-Quraysh waliifahamu kwa njia ya Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah. Yeye ameifahamu kwa njia ya Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah.
Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah ni kitu kipo. Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah ipo kwa watu na hakuna walioipinga isipokuwa watu wenye kudhihirisha kuwa wanapinga. Vinginevyo ndani ya nafsi zao wanajua kuwa hakuna muumba, mruzukaji na mwenye kuyaendesha mambo isipokuwa Allaah. Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah ni kitu cha kimaumbile. Hakuna yeyote mwenye kuikanusha. Ingelikuwa inatosheleza basi kusingelikuwa na haja ya kutumilizwa Mitume (Swalla Allaahu ´alayhim wa sallam). Kila Mtume alikuwa akiwaambia watu wake:
لَقَدْ أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوْمِهِ فَقَالَ يَا قَوْمِ اعْبُدُوا اللَّـهَ
“Kwa hakika Tulimpeleka Nuuh kwa watu wake akasema: “Enyi watu wangu! Mwabuduni Allaah.” (07:59)
وَمَا أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ مِن رَّسُولٍ إِلَّا نُوحِي إِلَيْهِ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنَا فَاعْبُدُونِ
“Na Hatukutuma kabla yako Mtume yeyote isipokuwa Tulimfunulia Wahy ya kwamba: “Hakika hakuna mungu wa haki ila Mimi, basi niabuduni.”” (21:25)
Hakusema wakubali uola kwa sababu hiki ni kitu kilichopo. Jengine ni kwa sababu haitoshelezi.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Qaa´idah Jaliylah fiyt-Tawassul wal-Wasiylah (21) http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2137
- Imechapishwa: 09/07/2020
Swali: Mwenye kupeleka maana ya “Laa ilaaha illa Allaah” katika Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah na al-Haakimiyyah anazingatiwa ni miongoni mwa wale ambao makafiri wa ki-Quraysh ni wenye ufahamu zaidi yake?
Jibu: Bila ya shaka yoyote. Makafiri wa ki-Quraysh waliifahamu kwa njia ya Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah. Yeye ameifahamu kwa njia ya Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah.
Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah ni kitu kipo. Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah ipo kwa watu na hakuna walioipinga isipokuwa watu wenye kudhihirisha kuwa wanapinga. Vinginevyo ndani ya nafsi zao wanajua kuwa hakuna muumba, mruzukaji na mwenye kuyaendesha mambo isipokuwa Allaah. Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah ni kitu cha kimaumbile. Hakuna yeyote mwenye kuikanusha. Ingelikuwa inatosheleza basi kusingelikuwa na haja ya kutumilizwa Mitume (Swalla Allaahu ´alayhim wa sallam). Kila Mtume alikuwa akiwaambia watu wake:
لَقَدْ أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوْمِهِ فَقَالَ يَا قَوْمِ اعْبُدُوا اللَّـهَ
“Kwa hakika Tulimpeleka Nuuh kwa watu wake akasema: “Enyi watu wangu! Mwabuduni Allaah.” (07:59)
وَمَا أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ مِن رَّسُولٍ إِلَّا نُوحِي إِلَيْهِ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنَا فَاعْبُدُونِ
“Na Hatukutuma kabla yako Mtume yeyote isipokuwa Tulimfunulia Wahy ya kwamba: “Hakika hakuna mungu wa haki ila Mimi, basi niabuduni.”” (21:25)
Hakusema wakubali uola kwa sababu hiki ni kitu kilichopo. Jengine ni kwa sababu haitoshelezi.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Qaa´idah Jaliylah fiyt-Tawassul wal-Wasiylah (21) http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2137
Imechapishwa: 09/07/2020
https://firqatunnajia.com/makafiri-wa-quraysh-ni-wajuzi-zaidi-kuliko-watu-hawa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)