Maelezo ya Hadiyth “Hakika katika ufasaha kuna uchawi”

 5- al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kupitia kwa Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ambaye ameeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Hakika katika ufasaha kuna uchawi.”

Kwa sababu mtu mwenye ufasaha anaweza kuwaroga watu kwa usulubu na ufasaha wake. Huenda akawababaisha. Huenda akawahadaa na wasibainikiwe na ukweli wa mambo. Wengi wanasema kuwa Hadiyth inasifia ufasaha ikiwa inahusiana na haki. Wengine wanasema kuwa ufasaha unasemwa vibaya, kama alivosema Ibn ´Abdil-Barr kutoka kwa baadhi ya wanachuoni. Lakini hata hivyo ufasaha ikiwa unahusiana na haki na kulingania katika Qur-aan na Sunnah basi ni wenye kusifiwa kama ambavyo ni wenye kusemwa vibaya ikiwa utatumiwa katika kuhadaa na kuwababaisha watu. Hadiyth inaweza kuwa na maana zote mbili. Qur-aan na Sunnah vimekuja kwa ubainisho wa wazi na ufasaha katika kubainisha haki na kuwaita watu katika haki hiyo. Kuna mtu aliyekhutubu kwa ufasaha kabisa mbele na wakati wa ´Umar bin ´Abdil-´Aziyz ambapo akasema:

“Huu ni uchawi halali.”

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Kitaab-it-Tawhiyd, uk. 93
  • Imechapishwa: 26/01/2020