Ni nani anayewaongelea watawala wa Kiislamu wanaokhalifu dini? Tofauti baina ya sisi na nyinyi, ni kuwa sisi sio walinganizi wa fitina na wala hatulinganii katika uasi wala mapinduzi. Lakini nyinyi, ni kama alivyosema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

“Akipewa anaridhika, na kama hakupewa hukasirika.”

Akiwapa ´Aliy ´Abdullaah Swaalih mnaita watu kumpigia kura. Na kama hawapi, mnasema na kumwita Ba´thiy na kuwa mtamfanyia uasi na mapinduzi. Yote haya ni maneno ya kijinga.

  • Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.muqbel.net/sounds.php?sound_id=33 Tarehe: 1420-12-18/2000-03-23
  • Imechapishwa: 09/04/2022