Swali: Je, ni kweli kwamba Maaturiydiyyah na Ashaa´irah ni katika Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah?

Jibu: Sio katika Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah. Bali Maaturiydiyyah, Ashaa´ira na Mu´tazilah ni mapote yenye kujitegemea. Lakini pote lililo karibu kidogo na Ahl-us-Sunnah ni Ashaa´irah. Wamethibitisha sifa saba na wakapindisha maana zengine zilizobaki. Ahl-us-Sunnah wao wanathibitisha majina na sifa zote za Allaah. ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-RaajihiyAshaa´irah wao wanathibitisha sifa saba. Baadhi yao wanathibitisha sifa ishirini. Wengine wanathibitisha arobaini. Mu´tazilah wamekanusha sifa zote na hawakuthibitisha isipokuwa majina peke yake. Jahmiyyah wamekanusha majina na sifa. Ndio maana wanachuoni wamewakufurisha. Baadhi ya wanachuoni wamewakufurisha Jahmiyyah moja kwa moja, wengine wamewafanyia Tabdiy´ na wengine wamewakufurisha wale wenye kuchupa mipaka katika wao.

´Allaamah Ibn-ul-Qayyim ametaja katika shairi lake “ash-Shaafiyah” kwamba kuna wanachuoni 500 waliowakufurisha Jahmiyyah.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (14)
  • Imechapishwa: 14/06/2020