Swali: Qaz´ ni kunyoa baadhi ya nywele na kuacha zengine. Mtu akipunguza baadhi ya nywele, na asinyoe, kunazingatiwa pia kuwa ni Qaz´?

Jibu: Ndio. Ni Qaz´ pia. Ni mamoja amepunguza au amenyoa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Ima nyoa zote au ziache zote.”[1]

Kupunguza na kunyoa ni kitu kimoja.

[1] al-Muhallaa (7/211).

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Fath-il-Majiyd (71) https://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/fathul-majd18-02-1439h-01.mp3
  • Imechapishwa: 13/02/2021